FIKIRI ZA SIKU – Chapeo Ya Wokovu

FIKIRI 31; KINACHOKUFANYA USIJIAMINI.

Kitu kinapozidi kuwa changamoto kwako, inabidi ukae chini na ujiulize nini inakupelekea kuwa hivyo. Hii itakusaidia kurekebisha pale unapoona ndio chanzo ya yote. Ikiwa kwako changamoto kubwa ni kutojiamini, unapaswa kukaa chini na kufikiri nini huwa inakufanya usijiamini. Labda hujiamini kusimama mbele za watu, labda hujiamini kuongea mbele za watu kuwaeleza kile ambacho unatamani wakisikie [...]

By | April 7th, 2020|FIKIRI ZA SIKU|0 Comments

FIKIRI 30; UNAPOJIKUTA HUJISIKII AMANI.

Sio Mara zote kutojisikia vizuri au kutojisikia amani moyoni ni kwa sababu kuna watu wamekukosea. Sio kana kwamba umepewa taarifa mbaya, sio kana kwamba umekosa kazi, au fedha. Wakati mwingine hatuna amani mioyoni mwetu kwa sababu ya kuchezea muda wetu vibaya katika siku yetu tunayopewa na Mungu. Wakati mwingine ni kwa sababu ya kutowajibika vizuri [...]

By | March 24th, 2020|FIKIRI ZA SIKU|0 Comments

FIKIRI 29; UKIPEWA UNAWEZA?

Mtu anaweza akawa na malalamiko fulani, malalamiko ambayo yanaonyesha kunyimwa kitu, au kunyimwa nafasi. Malalamiko ambayo mtu mwingine akimsikiliza, na huyo mtu anayemsikiliza akawa hamjui vizuri. Akamsikiliza bila kusikiliza upande wa pili unaolalamikiwa, mtu huyo anaweza kuona kweli anachosema huyo mtu. Na yupo anachosema kuhusu jambo fulani labda la kunyimwa nafasi au kitu, anachosema ni [...]

By | March 23rd, 2020|FIKIRI ZA SIKU|0 Comments

FIKIRI 28; UNAUMIA KWA KUONEWA.

Unafikiri unavyoumia ni kwa sababu ya kuonewa au ni kwa sababu ya uelewa wako wa mambo ulivyo. Kauli hii inaweza isiwe njema sana kwako ila ndio ukweli wenyewe ulivyo. Inawezekana kabisa hilo unaloona umeonewa sio kweli umeonewa isipokuwa ni vile uelewa wako ulivyo. Ama inawezekana kabisa kwa kutojua kwako neno la Mungu linasemaje kuhusu hilo, [...]

By | March 6th, 2020|FIKIRI ZA SIKU|0 Comments

FIKIRI 27; WATAKAPOKUSIKILIZA.

Watu wengi tunapenda kuona wengine wakitusikiliza kwa makini, wakifanyia kazi yale tunawaambia wayafanye, wakifuata ule ushauri tunawashauri. Pamoja na kutamani huko bado kuna watu hatupati nafasi hiyo ya kusikilizwa, mtu anaweza akawa anaongea asipewe usikivu wowote na wale anaowalenga. Achana na ule utulivu wa kulazimisha wengine watulie na kukusikiliza, watu wenyewe wakiwa wanajua una kitu [...]

By | March 4th, 2020|FIKIRI ZA SIKU|0 Comments

FIKIRI 26; WATAKAPOSOMA ULICHOANDIKA.

Sio jambo la kuficha, wala sio jambo la kuonea aibu kusema hadharani, ipo wazi kabisa kuwa wengi wetu ni wavivu/wazembe wa kusoma makala ndefu iliyoandikwa. Hiyo ni makala, ukimpeleka mtu kwenye usomaji wa vitabu huko ndio unampoteza kabisa. Ataona kama umempeleka sehemu ambayo ni mateso makubwa kwake. Hilo utakubaliana nami hasa sisi Watanzania, japo sio [...]

By | March 3rd, 2020|FIKIRI ZA SIKU|0 Comments

FIKIRI 25; INAVYOTAKIWA…

Kabla ya kulalamika jiulize haya; Je umefanya kazi kama inavyotakiwa? Je umejituma kama inavyotakiwa? Je umekaa kwenye nafasi yako inavyotakiwa? Je umetunza maisha yako ya ujana kama inavyotakiwa? Je umetunza maisha yako ya wokovu kama inavyotakiwa? Hebu fikiri tu mwenyewe, kabla hujaanza kulaumu/kuwalalamikia wengine, kabla hujaanza kuwatupia wengine lawama. Una uhakika umefanya ipasavyo kwa sehemu [...]

By | February 23rd, 2020|FIKIRI ZA SIKU|0 Comments

FIKIRI 24; UKIMSIFIA…

Mtu akifanya vizuri ni vizuri akapewa hongera zake, au ni vizuri ukamsifia kutokana na jambo jema alilolifanya. Ama kutokana na kazi yake njema, ama kutokana na bidii yake njema. Vibaya sana kukaa na sifa njema ya mtu bila kumwambia, na wakati una uwezo wa kumweleza vile anajitoa, vile anafanya vizuri. Sasa wengine huwa tunasubiri mtu [...]

By | February 21st, 2020|FIKIRI ZA SIKU|0 Comments

FIKIRI 23; MITANDAO YA KIJAMII.

Nikizungumza mitandao ya kijamii sio jambo geni kwenye masikio yetu, ni jambo ambalo linaeleweka kwa watu wengi sana. Hata yule ambaye hatumii hii mitandao ya kijamii anaijua, watu wengi sana ananunua simu anatamani awe mmoja wa wale waliopo Facebook, instagram, WhatsApp, Twitter, LinkedIn, YouTube nk. Napenda nikufikirishe leo, tangu umejiunga au tangu umeifahamu mitandao ya [...]

By | February 20th, 2020|FIKIRI ZA SIKU|0 Comments

FIKIRI 22; SIFA ZIPI UNAPENDA UWE NAZO.

Naamini kila mmoja wetu anapenda awe na sifa fulani njema katika maisha yake, na kama kuna mtu hapendi sifa njema basi atakuwa anahitaji msaada wa kiroho. Lakini wengi wetu tunapenda tuwe na sifa fulani njema, na sifa hizo sio za kuigiza, sifa ambazo zinaendana na yale maisha yetu tunaishi. Sifa zinazotoka ndani yetu, ambazo hufanyi [...]

By | February 19th, 2020|FIKIRI ZA SIKU|0 Comments

Watch Dragon ball super