Neno La Leo – Chapeo Ya Wokovu

Tunaongozwa Na Roho Mtakatifu Kunena Yaliyotoka Kwa Mungu

"Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu", 2 Pet 1:21 SUV. Petro anatuthibitishia wazi asili ya Kimungu na mamlaka yake ya unabii kwenye Maandiko Matakatifu. Waamini wote wanapaswa kuwa na mtazamo usiobadilika kuhusu maandiko matakatifu yaliyovuviwa na yaliyojaa mamlaka ya Kimungu. Ukishasoma neno [...]

By | March 18th, 2023|Neno La Leo|0 Comments

Usiwe Na Tamaa Ya Fedha Ukitaka Kumtumikia Mungu Vizuri

"Lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia, si kwa kulazimishwa, bali kwa hiari kama Mungu atakavyo; si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo", 1 Pet 5:2 SUV. Ukiwa mtumishi wa Mungu na kiongozi wa kanisa unapaswa kujihadhari na mambo mawili hatari; Kupenda Fedha, moja ya kanuni katika agano jipya kwa waangalizi au [...]

By | March 17th, 2023|Neno La Leo|0 Comments

Uhuru Wetu Hauturuhusu Kutenda Dhambi

"Ishini kama watu huru, lakini msitumie uhuru wenu kama kisingizio cha kutenda uovu, bali ishini kama watumishi wa Mungu", 1 Petro 2:16 NEN. Moja ya mambo muhimu sana kufahamu ni hili, wapo baadhi ya watu wametumia neno la Mungu vibaya. Uhuru tulionao katika Kristo sio uhuru wa kufanya mabaya, sio uhuru wa kufanya tunachojisikia. Tunaweza [...]

By | March 14th, 2023|Neno La Leo|0 Comments

Tunalindwa Na Nguvu Za Mungu Kwa Njia Ya Imani

"Nanyi mnalindwa na nguvu za Mungu kwa njia ya imani hata mpate wokovu ulio tayari kufunuliwa wakati wa mwisho", 1 Pet 1:5 SUV. Petro anatupa ujumbe muhimu sana kwa mwamini vile tunalindwa na nguvu za Mungu na tunavyoweza kuwa salama. Ukiwa mwamini unalindwa na nguvu za Mungu dhidi ya majeshi ya pepo wabaya, ambayo yanaweza [...]

By | March 13th, 2023|Neno La Leo|0 Comments

Mrejeshe Kwenye Njia Sahihi Yule Aliyerudi Nyuma Kiimani

"Ndugu zangu, ikiwa mtu wa kwenu amepotelea mbali na kweli, na mtu mwingine akamrejeza; jueni ya kuwa yeye amrejezaye mwenye dhambi hata atoke katika njia ya upotevu, ataokoa roho na mauti, na kufunika wingi wa dhambi", Yak 5:19‭-‬20 SUV. Moja ya kazi kubwa ambayo tunapaswa kuifanya waamini ni kufanya kila linalowezekana kuhakikisha wale waliopotoka katika [...]

By | March 11th, 2023|Neno La Leo|0 Comments

Usijivune Kupitiliza Kwa Mafanikio Uliyopata Ukaona Wengine Hawajitumi

"Lakini sasa mwajisifu katika majivuno yenu; kujisifu kote kwa namna hii ni kubaya", Yak 4:16 SUV. Wapo watu huweka malengo yao makubwa na wakafanikiwa kuyatimiza kama walivyopanga, jaribu linalowapata watu hawa ni majivuno. Majivuno haya huwajengea dhana potofu na ya uongo kuwa kufanikiwa kwao ni kwa akili zao na juhudi zao binafsi. Husahau kabisa kuwa [...]

By | March 11th, 2023|Neno La Leo|0 Comments

Tahadhari Muhimu Kwa Walimu Wa Neno La Mungu

"Ndugu zangu, wengi wenu msiwe waalimu. Kama mjuavyo, sisi waalimu tutapata hukumu kubwa zaidi kuliko wengine", Yakobo 3:1 BHN. Kujitoa na kuanza kufundisha watu linaweza likawa jambo jepesi kwa mtu anayejisikia kufanya hivyo na akafundisha jambo analoona yeye. Kazi ya walimu wengine wanaweza kuona tabu kufundisha kutokana na vipengele vyake vilivyokaa vya ufundishaji. Tunapozungumza kuhusu [...]

By | March 9th, 2023|Neno La Leo|0 Comments

Chimba Ukate Mizizi Na Shina La Uchungu Ndani Yako

"Mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo", Ebr 12:15 SUV. Shina la uchungu humaanisha roho na hali ya uhasama na chuki kali iliyo ndani ya mtu. Hali hii inaweza ikawa kumwelekea Mungu au iliyosababishwa na matendo mabaya aliyotendewa mtu. Uchungu husababishwa [...]

By | March 4th, 2023|Neno La Leo|0 Comments

Mwenye Haki Wa Mungu Ataishi Kwa Imani

"Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye", Ebr 10:38 SUV. Moja ya kanuni muhimu kwa mwamini na iliyothibitishwa na maandiko matakatifu ni hii ya Imani, ukisoma Habakuki 2:4, Warumi 1:17, Wagalatia 3:11, Waebrania 10:38 utaona Imani inazungumzwa sana kwa mwamini. Pasipo Imani hatuwezi kumpendeza Mungu, Imani hutufanya tuwe [...]

By | March 2nd, 2023|Neno La Leo|0 Comments

Mungu Habadiliki Na Hawezi Kusema Uongo

"Ili kwa vitu viwili visivyoweza kubadilika, ambavyo katika hivyo Mungu hawezi kusema uongo, tupate faraja iliyo imara, sisi tuliokimbilia kuyashika matumaini yale yawekwayo mbele yetu", Ebr 6:18 SUV. Moja ya sifa kuu aliyonayo Mungu wetu ni habadiliki na hana ahadi za uongo, lile aliloliahidi kwetu kupitia neno lake atalitimiza sawasawa na mapenzi yake. Mtu anaweza [...]

By | February 25th, 2023|Neno La Leo|0 Comments

Watch Dragon ball super