Neno La Leo – Chapeo Ya Wokovu

Uongozi Wa Kulaumiwa Kwa Mazuri Uliyofanya Na Kuwachukulia Hatua Kali Wale Waliokosea

‭‭Hes‬ ‭16:12‭-‬13‬ ‭SUV‬‬[12] Kisha Musa akatuma kuwaita Dathani na Abiramu, wana wa Eliabu; nao wakasema, Hatuji sisi; [13] je! Ni jambo dogo, wewe kutuleta kutoka nchi iliyojawa na maziwa na asali, ili kutuua jangwani, lakini pamoja na haya wajikuza mwenyewe uwe mkuu juu yetu kabisa? Hawa ndugu Dathani na Abiramu kumgomea Musa na kumhoji mambo [...]

By | September 27th, 2023|Neno La Leo|0 Comments

Mali Uliyonayo Au Vitu Unavyomiliki Si Vyako Vina Mwenyewe

"Nayo nchi haitauzwa kabisa kabisa; kwani nchi ni yangu mimi; maana ninyi ni wageni na wasafiri wangu", Law 25:23 SUV. Mungu aliwaambia Waisraeli bila kuwaficha hili, kuwa ardhi waliyokuwa nayo haikuwa miliki yao, yaani hawakuwa wamiliki wakuu, bali yeye ndiye alikuwa mmiliki wa ardhi hiyo. Kama ilivyo Sheria ya Tanzania, mwenye ardhi haswa ni Serikali, [...]

By | September 6th, 2023|Neno La Leo|0 Comments

Weka Akiba Yako Kwa Ajili Ya Kuwagawia Wasiojiweza/Maskini

"Nanyi hapo mtakapovuna mavuno ya nchi yenu, usivune kabisa kabisa pembe za shamba lako, wala msiyakusanye masazo ya mavuno yako; utayaacha kwa ajili ya huyo maskini, na mgeni; mimi ndimi BWANA, Mungu wenu", Law 23:22 SUV. Waisraeli walipaswa kutovuna mazao yote ya shamba walilolima, walipaswa kubakisha mavuno yao shambani kwa ajili ya maskini na wageni. [...]

By | September 4th, 2023|Neno La Leo|0 Comments

Mpende Mgeni/ndugu Unayekaa Naye Nyumbani Kwako

"Mgeni akaaye pamoja nawe atakuwa kama mzalia kwenu; mpende kama nafsi yako; kwa maana ninyi mlikuwa wageni katika nchi ya Misri; Mimi ndimi BWANA, Mungu wenu", Law 19:34 SUV. Tuna ndugu mbalimbali tunaweza kuwapokea kwenye nyumba zetu na kuanza kuishi nao, watu ambao wanakuwa sehemu ya familia zetu. Watu hawa wanaoingia katika familia zetu, wanaweza [...]

By | August 30th, 2023|Neno La Leo|0 Comments

Namna Mungu Anavyojali Afya Zetu Sio Vile Tunavyochukulia Baadhi Yetu

Mtu ye yote atakayekigusa kitanda chake huyo, atazifua nguo zake, na kuoga mwili wake majini, naye atakuwa najisi hata jioni. Law 15:5 SUV. Najisi hii nimeanza kuiona kwa namna ya pekee sana tangu nianze kusoma kitabu hichi cha Walawi, pamoja na makatazo haya yalikuwa mtu akifanya alichokatazwa atakuwa amejipatia hatia mbele za Mungu. Haikuwa Dhambi [...]

By | August 25th, 2023|Neno La Leo|0 Comments

Katazo La Vyakula Najisi Na Utakatifu Wa Mwamini Siku Za Leo

“Msifanye nafsi zenu kuwa ni chukizo kwa kitu cho chote chenye kutambaa, kitambaacho, wala msifanye nafsi zenu kuwa ni najisi kwa vitu hivyo, mkajipatia uchafu kwa hivyo. Kwa kuwa mimi ni BWANA, Mungu wenu; takaseni nafsi zenu basi; iweni watakatifu, kwa kuwa mimi ni Mtakatifu; wala msitie uchafu nafsi zenu kwa kitu kitambaacho cha aina [...]

By | August 21st, 2023|Neno La Leo|0 Comments

Madhara Ya Kufanya Mambo Kinyume Na Mungu Alivyokuagiza

“Na Nadabu na Abihu, wana wa Haruni, wakatwaa kila mtu chetezo chake, wakatia moto ndani yake, wakatia na uvumba, nao wakatoa moto wa kigeni mbele ya BWANA, ambao yeye hakuwaagiza. Kisha moto ukatoka hapo mbele za BWANA, nao ukawala, nao wakafa mbele za BWANA”, Law 10:1‭-‬2 SUV. Ibada za kikuhani zilivyoanza hemani mwa Bwana, watoto [...]

By | August 19th, 2023|Neno La Leo|0 Comments

Mjue Kuhani Wa Agano La Kale Na Wa Agano Jipya Na Kazi Zake

"Mtwae Haruni, na wanawe pamoja naye, na yale mavazi, na mafuta ya kutia, na ng’ombe mume wa sadaka ya dhambi, na kondoo waume wawili, na kikapu cha mikate isiyotiwa chachu; kisha ukutanishe mkutano wote hapo mlangoni pa hema ya kukutania", Law 8:2‭-‬3 SUV. Sura ya leo ya 8 tunaona imejikita zaidi kuelezea kusimikwa kwa Haruni [...]

By | August 17th, 2023|Neno La Leo|0 Comments

Umhimu Wa Ibada Kwa Mwamini Mwenye Nia Ya Kumpendeza Mungu

"Wataichinja sadaka ya hatia pale pale waichinjapo sadaka ya kuteketezwa; na damu yake atainyunyiza katika madhabahu pande zote", Law 7:2 SUV. Agano la kale ibada za Waisraeli zilikuwa njia ya mawasiliano kati ya Mungu na wao, ibada ambazo ziliwafanya wasikie Mungu anasema nini juu ya maisha yao. Ibada hizi zilikuwa za maombi yaliyoonyesha toba mbele [...]

By | August 16th, 2023|Neno La Leo|0 Comments

Usimdhulumu Mtu Vitu Vyake Mlivyopeana Kwa Makubaliano Maalumu

"Mtu awaye yote akifanya dhambi, na kuasi juu ya BWANA, akamdanganya mwenziwe katika jambo la amana, au la mapatano, au la kunyang’anya, au kumwonea mwenziwe", Law 6:2 SUV. Waisraeli waliagizwa kutonyang'anyana vitu, kutodhulumiana, kwa yale waliyopeana kwa kupatana kurejesheana. Mtu yeyote aliyeenda kinyume na hayo alihesabika ametenda dhambi, na alipaswa kurudisha hicho kitu alichomdhulumu mwenzake, [...]

By | August 15th, 2023|Neno La Leo|0 Comments

Watch Dragon ball super