“Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja”, 2 Pet 3:8 SUV.
Mtazamo wetu na wa Mungu unaweza kupishana tusipoelewa, yapo mambo tunayatazama kutokana na tulivyozoea mazingira yetu.
Tukija katika suala la muda, Mungu hutazama muda kwa mtazamo wa umilele.
“Maana miaka elfu machoni pako Ni kama siku ya jana ikiisha kupita, Na kama kesha la usiku”, Zab 90:4 SUV.
Biblia inapozungumzia miaka elfu moja mtazamo upo hivi, inaonekana tofauti kwa Mungu kuliko kwa wanadamu.
Mungu anaweza kutimiza jambo ambalo sisi tunaona lingechukua miaka elfu moja kutimia.
Wakati mtazamo wetu unatuonyesha jambo litatimia siku moja, Mungu anaweza kulitimiza kwa miaka elfu moja.
Hii inatupa kufahamu kuwa hatupaswi kuwa na mtazamo nje na neno la Mungu, mitazamo yetu ikienda kinyume na neno la Mungu mambo yetu yatakuwa tofauti.
Hatupaswi kumchukulia Mungu vile tunaona sisi, maana mambo yetu yatakuwa tofauti na tutaona Mungu hayupo au anasema uongo.
Soma neno ukue kiroho
Liwe jua iwe mvua soma biblia yako
Mungu akubariki sana
Samson Ernest