“Ishini kama watu huru, lakini msitumie uhuru wenu kama kisingizio cha kutenda uovu, bali ishini kama watumishi wa Mungu”, 1 Petro 2:16 NEN.
Moja ya mambo muhimu sana kufahamu ni hili, wapo baadhi ya watu wametumia neno la Mungu vibaya.
Uhuru tulionao katika Kristo sio uhuru wa kufanya mabaya, sio uhuru wa kufanya tunachojisikia.
Tunaweza kufikiri tumewekwa uhuru hakuna chochote kinachotufunga tusitende tunavyojikia kutenda.
Uhuru wetu una mipaka, mipaka hii ni kati ya wema na ubaya.
Tumewekewa ukuta ili tusiweze kuvuka kwenye upande wa mabaya, tunapaswa kuishi kwenye eneo linalompendeza Mungu wetu.
Kosa kuona umewekwa huru katika Kristo ukaanza kufanya mambo yasiyofaa kwa kigezo kuwa umewekwa huru.
Uhuru unaosemwa hapa ni kufunguliwa kutoka katika kifungo cha Shetani, na kuingia katika ufalme wa Mungu.
Utumwa aliokuwa nao mtu, siku anapomwamini Yesu anawekwa huru wakati huo.
Anapowekwa huru anapaswa kulinda nafasi hiyo kwa kutomtenda Mungu dhambi ili ulinzi wake uendelee kuwa pamoja naye.
Tunapoenda kuhitimisha unapaswa kuelewa kuwa hatupo huru kumtenda Mungu dhambi, tupo huru kumtukuza Yesu katika maisha yetu.
Soma neno ukue kiroho
Liwe jua iwe mvua soma biblia yako
Mungu akubariki sana
Samson Ernest