Mahusiano – Chapeo Ya Wokovu

Je, Mungu Akiamua Kutoa Ushahidi Wake Kwako Utabaki Salama Au Utahukumiwa?

"Nena na wana wa israeli, uwaambie, kama mke wa mtu ye yote akikengeuka, na kumkosa mumewe, na mtu mume akalala naye kwa uasherati, na jambo hilo likamfichamania mumewe, likawa jambo lisilojulikana, na huyo mwanamke akawa najisi, wala hapana shahidi aliyeshuhudia juu yake, wala hakufumaniwa", Hes 5:12‭-‬13 SUV. Uliwekwa utaratibu kwa Waisraeli, yule mwanaume ambaye alimdhania [...]

By | September 14th, 2023|Mahusiano|0 Comments

Sababu 10 Zinazopelekea Mahusiano Ya Uchumba Kuvunjika Mara Kwa Mara Kwa Mtu

"Huyu wa safari hii akikuacha usikubali kuachwa kizembe, mpeleke police apigwe virungu kwanza akili imuingie kisawasawa" SK. Katika kundi la wasap la Singles Talk-CYW ndugu mmoja alitoa kauli hii kama utani, lakini ndani yake kulikuwa na ujumbe wa muhimu sana, ilionyesha kuna changamoto kwenye eneo hili. Vijana wengi wanaanzisha mahusiano ila hayafikii lengo yanavunjikia njiani. [...]

By | July 12th, 2023|Mahusiano|0 Comments

Mambo 10 Muhimu Ya Kukusaidia Kupata Mwenzi Wako Sahihi Wa Maisha Yako

"Bali enenda hata nchi yangu, na kwa jamaa zangu, ukamtwalie mwanangu Isaka mke", Mwa 24:4 SUV. Kwa kujua umhimu wa Isaka kupata mke sahihi, ili aweze kuendana na yale ambayo Mungu alishamjulisha Ibrahimu, Ibrahimu alimwagiza msaidizi wake wa kazi kwenda kumtafutia mwanaye mke wa kuoa. Mashaka makubwa yalikuwa kwa mtumishi huyu wa Ibrahimu ila alimwondoa [...]

By | June 21st, 2023|Mahusiano|0 Comments

Je Unayemwomba Akupe Mke/mume Mwema Una Uhusiano Naye Mzuri?

"Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu", 1 Pet 1:15‭-‬16 SUV. Kuna mazungumzo au hoja au jumbe huwa hatuzipendi sana kuzisikia kwenye masikio yetu, zaidi huwa tunapenda kusikia jumbe fulani nzuri za kututia moyo, sio vibaya kabisa ila [...]

By | May 16th, 2023|Mahusiano|0 Comments

Je Ni Sahihi Wachumba Kufungua Biashara Ya Pamoja Kwa Kuchangishana Fedha?

"Hivi ni sahihi wachumba kufanya miradi ya pamoja hasa ya biashara na wanaweza kukopeshana pesa?" Aruba L. Hili ni swali la ndugu ameuliza, kwa faida ya watu wote tunaweza kulijibu ili kila mmoja apate faida ya majibu ya swali hili ambalo baadhi ya vijana hujiuliza hasa upendo unapokuwa juu. Uchumba ni hatua muhimu sana na [...]

By | May 9th, 2023|Mahusiano|0 Comments

Mungu Anakupa Msaidizi Wa Kufanana Naye

"BWANA Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye", Mwa 2:18 SUV. Moja ya jambo muhimu sana aliliona Mungu baada ya kumpa Adamu majukumu ya kuitunza Bustani ya Edeni, aliona sio vyema aendelee kuwa peke yake akamfanyia msaidizi wa kufanana naye. Hii inatupa picha kuwa tangu mwanzo Mungu aliifanya [...]

By | April 27th, 2023|Mahusiano|0 Comments

Njia Rahisi Ya Kumvuta Mume Wako Kwenye Maisha Ya Wokovu

"Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno", 1 Pet 3:1 SUV. Petro anatoa fundisho kwa mwanamke aliyeolewa na aliyepata neema ya wokovu wakiwa kwenye ndoa. Anapaswa awe na ushawishi kupitia matendo yake, ili aweze kumvuta mume wake asiyeamini aweze kuokoka. Moja ya [...]

By | March 15th, 2023|Mahusiano|0 Comments

Zinaa Sio Ya Kuifurahia Na Kuimbilia Kuifanya

"Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe", 1 Kor 6:18 SUV. Zipo dhambi nyingi zilizo chukizo mbele za Mungu, lakini hizi dhambi zinatofautiana katika utendaji wake na viwango vyake. Zinaa ina utofauti na dhambi zingine, hili ni tendo ambalo humchukiza [...]

By | December 5th, 2022|Mahusiano|0 Comments

Jenga Mtazamo Sahihi Juu Ya Wanaume/Wanawake Kabla Hujaoa/Hujaolewa

Tuingie moja kwa moja kwenye mada tajwa hapo juu, watu baadhi wameingia kwenye ndoa na watu sahihi ila mitazamo yao juu yao sio sahihi, wapo wameingia kwenye ndoa sio sahihi kwa sababu ya mitazamo yao isiyo sahihi, na wapo hawataki kuingia kwenye ndoa wamebaki kutangatanga na kila mwanaume/mwanamke kwa sababu ya mitazamo yao mibaya. Mtu [...]

By | August 23rd, 2022|Mahusiano|0 Comments

Usitishwe Na Uchakavu Wa Nje Wa Anayetaka Kukuoa Au Unayetaka Kumuoa

Vijana wengi au watu wengi hili hulipuuza na kutazama hali nzuri ya anayetaka kumuoa au kuolewa naye. Mara nyingi nimekuwa nikiwaambia vijana, "kuna dhahabu zimejificha kwenye tope", hadi kuibaini unahitaji uwe na utulivu wa kiroho na uwe na mahusiano mazuri na Mungu. Wapo wanaume au wanawake, ukimwona kwa jicho la nyama na hali aliyonayo au [...]

By | August 16th, 2022|Mahusiano|0 Comments

Watch Dragon ball super