
Yesu asifiwe mwana wa Mungu, umewahi kukaa na kufikiri kile unachojifunza ndani ya Biblia au ndani ya sura ya siku unayosoma.
Kile unaandika ambayo tunaiita ni tafakari yako, je kinafanana kweli na ulichojifunza?
Acha kufanana na ulichojifunza, je umewahi kukaa chini na kufikiri unachoandika kinasomwa na watu 100?
Acha kusomwa tu na watu 100, je wakisoma kuna kitu wanajifunza kupitia tafakari yako?
Na kama wanajifunza kitu, je ni kweli walipaswa kujifunza kwa kiwango hicho?
Hebu fikiri mwenyewe tu, uone kweli wewe ni wa kufanya hivyo? Kisha chukua hatua.
Mungu akubariki sana.
Ndugu yako katika Kristo,
Samson Ernest.
www.chapeotz.com