KUVUMA KWA MUDA.
Haleluya, nakusalimu katika jina la Bwana wetu YESU Kristo aliye hai. Nafasi nyingine tena tumeipewa na Mungu wetu, tukiwa hai, uhai huu tunapaswa kuutumia vyema ili kuleta faida kwake.
Leo tuzungumzie kuhusu kuvuma kwa wengi wetu na kupotea, imekuwa ni tabia ya kawaida kuanzisha mambo mazuri ya kumtukuza Mungu wetu. Lakini baada ya muda fulani tunasahaulika kabisa kama tuliwahi kufanya hilo jambo.
Wengi wetu inabaki story, nilikuwaga msomaji wa NENO la MUNGU sana, nilikuwaga muimbaji mzuri sana, nilikuwa mhudhuriaji mzuri sana wa ibada, nilikuwa mwombaji mzuri sana.
Mtu huyu si kana kwamba amezeeka sana na hawezi kufanya hivyo vitu tena, la hasha! Amekaukiwa, sasa amebaki kujikumbusha yale ya zamani wakati hapo alipo amechoka na hachukui hatua yeyote.
Kuvuma kama upepo katika huduma na kupotelea mbali, haiwezi kutufanya sisi tuwe vizuri bali inatutambulisha kuwa tuna hali mbaya KIROHO.
Ulivyokuwa na mahusiano mazuri na Mungu huko nyuma, lakini sasa hayo mahusiano hayapo tena, fahamu haiwezi kukufanya ukaitwa mwana wa Mungu, bali utaitwa mwana mpotevu.
Jifunze kutokuwa mtu wa kuvuma kama upepo alafu ukishapita unasahaulika kama ulikuwepo eneo lile, usiwe mtu wa kuanza na Mungu vizuri alafu ukapotelea gizani badala ya kuendelea kuimarika zaidi ya ulivyoanza.
Wengi tumeanza vizuri na Mungu, wengi tumeanza kujisomea vizuri Neno la Mungu, lakini baada ya muda tulizimika kama moto wa mabua. Yanabaki tu majivu, inakuwa haijulikani kilichoungua ni kitu gani.
Kitu gani kinatufanya tuvume kwenye mambo ya Mungu na kupotea? Ni kuleta mazoea na kuingiza ukawaida wa kumtafuta Mungu kwa bidii.
Hatuwezi kujifunza NENO la MUNGU kwa msimu fulani alafu tunaacha kabisa kusoma, lazima tuelewe tunapaswa kuongeza bidii kila wakati ili tuendelee kuona mabadiliko kiroho katika usomaji wetu.
Kusema nikuwaga unasoma Neno zamani alafu sasa hivi husomi, hilo ni tatizo ambalo limekugandamiza ili usiweze kuwa mwanafunzi mzuri wa YESU.
Ikiwa wewe ni mtumishi wa Mungu kwa njia ya uimbaji, unawezaje kutupa nyimbo zenye mguso wa Mungu. Ikiwa wewe mwenyewe huna NENO la MUNGU moyoni mwako, inakuwaje kuwazamisha wengine katika uwepo wa Mungu wakati wewe mwenyewe hujazama.
Tufike wakati tuache wokovu wa msimu, wokovu unaovuma na kupotea kabisa, ninaposema kupotea ni kusahaulika kwa mtu aliyekuwa anafanya huduma, inabaki tu wengine wakisimliwa fulani alikuwa hivi.
Tunapaswa kuelewa mambo ya rohoni hayapaswi kuchakaa, bali yanapaswa kufanywa upya kila siku, huwezi kufananisha kiwango cha mafanikio ya kimwili na kiroho. Inaweza isiogopeshe sana watu kusema alikuwa na pesa nyingi sana wakati ule, ila sasa hana kitu kwa sababu alifilisika.
Kufilisika kimwili haiwezi kukuzuia usione mbingu wala haiwezi kukuondolea mahusiano yako na Mungu, ila kufilisika kiroho ndugu yangu, ni mbaya kuliko yote. Ndio maana nimekuambia hatupaswi kuanza vizuri alafu tukapotelea mbali, kataa kabisa hicho kitu katika maisha yako.
Pale hatuwezi tena kutenda kazi ya Mungu kwa changamoto za uzee, ambao biblia imeutaja kama nyakati mbaya. Nyakati ambazo huwezi kula vizuri kwa shida ya meno, nyakati ambazo huwezi kusimama saa moja ukitoa huduma, nyakati ambazo huwezi kutembea tena umbali mrefu, nyakati ambazo huwezi kuomba vizuri kwa uzaifu wa mwili.
Hizo ndizo nyakati ambazo tunapaswa kujikumbusha mambo mazuri ya Mungu tuliyotenda katika ujana wetu, wakati ambao huna uwezo tena wa kuona vizuri maandiko Matakatifu kwa sababu macho hayawezi.
Sio una nguvu kabisa unasema nilikuwa vizuri miaka fulani wakati hapo ulipo umechoka vibaya kiroho, usiwe mtu wa kuvuma kama upepo na kupotelea mbali.
Ulikuwa msomaji mzuri wa NENO lakini umeacha, rudi upesi na si kusimulia watu. Acha kujifariji kwa uvumi wa zamani, Mungu haangalii mwanzo wako, anaangalia mwisho wako mwema.
Ulikuwa bado hujaanza kusoma NENO la MUNGU kwa visingizio vya hapa na pale, na sasa umejisikia ndani yako kuanza kusoma biblia. Na ulikuwa msomaji wa NENO la MUNGU lakini ulirudi nyuma, nikuombe uanze leo kusoma NENO.
Unaona kusoma peke yako pasipo kuwa na wenzako wa kukutia moyo, na unahitaji kuwa pamoja na wenzeko wenye nia moja na wewe. Unakaribishwa sana kwenye group la Wasap, tuma sms kwa njia ya wasap kwa namba hizo chini ili uungane na wenzeko katika kusoma na kutafakari Neno la Mungu kila siku.
Wale ambao tayari wapo group la Wasap, leo wapo kitabu cha 1 Nyakati 23, usipange kukosa hii.
Mungu akubariki sana.
Samson Ernest.
+255759808081.